Friday, August 26, 2011

Waasi wa Libya ni Hatari.

Waasi wa Libya wadhibiti kituo cha ukaguzi mpakani na Tunisia
muammar gaddafi
Wapiganaji waasi katika operesheni
Vikosi vya waasi wa Libya, vinaripotiwa kudhibiti kituo cha ukaguzi cha Ras Jdir kwenye mpaka wa Libya na Tunisia.
Vyanzo mbalimbali vya habari vimewanukuu mashahidi waliosema kuwa waasi wameudhibiti mpaka huo baada ya kupambana na wanajeshi wanaomuunga mkono kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.


Mpaka huo upo kwenye barabara muhimu ya pwani inayotokea Tunisia hadi Tripoli nchini Libya. Mwandishi habari wa DW Martin Fletcher alie Tripoli hivi sasa, anasema waasi wanafanya kila liwezekanalo kumkamata Gaddafi. Inadhaniwa kwamba Gaddafi amekimbilia mji alikozaliwa wa Sirte.
gaddafi bodyguards


Mji huo ulilengwa na ndege za kivita za NATO asubuhi ya hapo jana. Wakati huohuo Umoja wa Afrika umesema hautolitambua Baraza la Mpito la waasi kama chombo halali kinachowakilisha Libya, ilimradi mapigano yanaendelea nchini humo.

No comments:

Post a Comment