Wednesday, February 9, 2011

Twanga Pepeta waandaa varangati Valentine`s Day Tabata

Bendi ya African Stars maarufu kama Twanga Pepeta, itawatambulisha wanamuziki wake wapya kwenye onyesho lao litakalofanyika Siku ya Wapendanao kwenye ukumbi wa Da’ West Park, Tabata.
Onyesho hilo ambalo limeandaliwa na Bob Entertainment na kudhaniniwa na Dodoma Wine na Freditto Entertainment litajulikana kama Dodoma Wine Valentine Show.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Asha Baraka, alisema jana kuwa siku hiyo ya Februari 14 ambayo huadhimishwa na wapendanao duniani kote, watatumia kutambulisha wanamuziki wapya waliojiunga na bendi hiyo hivi karibuni wakiwemo wanenguaji.
Hata hivyo, Asha hakuwataja wanamuziki wala wanenguaji hao, lakini amesema kuwa wanatoka kwenye bendi mbalimbali maarufu nchini.
African Stars Entertainmernt (ASET) ni taasisi ya muziki ambayo kazi yake ni kuandaa na kukuza wanamuziki. Ninawaomba wapenzi wajitokeze kwa wingi siku hiyo ili waone silaha zetu mpya pamoja na rap zetu mpya,” alisema Asha.
Asha alisema pia wanamuziki wake wamejiandaa vya kutosha kuburudisha mashabiki wao siku hiyo.

No comments:

Post a Comment