Sunday, January 16, 2011
DALILI 10 ZA MWANAMKE ASIYEKUPENDA.
1 : Hataki kuambatana na wewe katika matembezi na kama ikiwa lazima anakuwa mtu wa masharti mara akuambie tangulia nakuja au kutembea nawe kwa mbali.
2: Anapata kigugumiza kukutambulisha kwa rafiki zake na jamaa zake.
3: Haonyeshi kubana matumizi kwa ajili ya maendeleo, kwake ni kufuja na kwenda mbele na huwa mfujaji mkubwa wa pesa na anapokosa kununa kabisa.
4: Anaahirisha kukutana na wewe mara kwa mara, tena bila kukueleza sababu za msingi, au kukutungia uongo wa dhahiri.
5: Anapokuwa akitoa maelezo ya mwanamme amtakaye sifa zake zinakuwa hazilingani na wewe, kwa mfano atakwambia napenda mwanamme mwenye mwili mkubwa , sifa ambazo wewe huna.
6: Hacheki kwa furaha, hata kama ukimchekesha haonyeshi furaha ya moyoni, ukimwambie twende tukatembee forodhani atakujibu ''Aaah, nimechoka mie nipo nyumbani'
7: Huwa hana wivu kabisa, hudiriki hata kukushawishi uwende Disco peke yako.
8: Hasamehe na kusahau, kosa la mwaka juzi analijengea hoja.
9: Humsisimui katika mambo ya faragha.
10: Mwepesi wa kutoa kauli ya TALAKA, ''kama vipi bora kila mtu akae kivyake vyake'' tena hataki kuambiwa ukweli na anapotokea akaambiwa hujitetea kwa kumtaja mwanaume mwingine '' Mbona Al-Udii (si jina halisi) anamfanyia hili , hamfanyii hivi mkewe''
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment